Nadumu Kwa Ahadi
1. Nadumu kwa ahadi zake Mfalme,
Yesu asifiwe kwa siku zote,
Nitamwimbia sana, atukuzwe
Kudumu kwa ahadi zake.
Ref
Dumu, dumu
Nadumu kwa ahadi za Bwana wangu
Dumu, dumu
Nadumu kwa ahadi za Mungu
2. Nadumu kwa ahadi, sina shaka,
Aahadi zisizokosa kabisa;
Kwa neno lake Mungu nitashinda;
Kudumu kwa ahadi zake.
3. Nadumu kwa ahadi, nafahamu
Nina utakaso mkamilifu;
Kudumu kwa uhuru wake Yesu,
Kudumu kwa ahadi zake.
4. Nadumu kwa ahadi zake Kristo,
Kwa milele nimefungwa na pendo;
Nitashinda kwa upanga wa Roho,
Kudumu kwa ahadi zake.
5. Nadumu kwa ahadi, sitakosa,
Sauti ya Roho nitasikia
Katika Mwokozi nimepumzika,
Kudumu kwa ahadi zake
Naendea msalaba
1. Naendea msalaba, Ni mnyonge, mpofu,
Yapitayo naacha nipe msalaba tu.
Ref
Nakutumaini tu, wee Mwana wa Mungu;
Nainamia kwako; Niponye sasa, Bwana.
2. Nakulilia sana: Nalemewa na dhambi;
Pole Yesu asema: “Nitazifuta zote.”
3. Natoa vyote kwako, nafasi nazo nguvu,
Roho yangu na mwili viwe vyako milele.
4. Kwa damu yake sasa amenivuta sana,
Upendo hubidisha, nimtafute Mwokozi.
5.Yesu yuaja tena! Nimepevuka kwake,
Kila chembe kamili; Msifuni yeye mponya!
Nakuapia Yesu
Nakuapia Yesu, kukutumikia
Wewe u mfunzi wangu na rafiki mwema.
Sitaogopa vita nikikufuata
Siipotezi njia, ukiniongoza.
Dunia i karibu, Bwana unilinde,
Na majaribu mengi, yako pande zote.
Adui siku zote, ni ndani na nje,
Ee Yesu univute, Karibu na wewe!
Nazisikia sauti, zenye tamaa mbaya,
Na mambo ya dunia, yanivuta sana.
Ee Bwana sema nami, Furaha iwe kuu,
Nitakusikiliza, Wewe mlinzi wangu.
Waagana na wote, wakufuatao,
Kwamba uliko wewe, nao watakuwa.
Nami ninaagana, kukutumikia,
Yesu nisaidie, kukuandamia.
Hatua zako Bwana, naziona wazi,
Nizikanyage vema, hapa duniani.
Nishike hata mwisho, Ee Yesu Mwokozi,
Nichukue nikifa, na kwako mbinguni.
Nakusalimu Kichwa
1. Nakusalimu kichwa kilichojaa damu,
Kilichovikwa taji la miiba mikubwa.
Kilichopata enzi kwa Mungu mbinguni,
kitukanwacho sasa matusi makali.
2. Bwana nayashukuru masumbuko yako,
Sababu ya kuteswa na kufa kuchungu.
Wewe umenishika nami nitakushika,
Mwisho nitakujia uliyenifia.
3. Nivike kama ngao nitakapo kufa,
Nione uso wako katika uchungu.
Ndipo nikutazame nikutumainie,
Anaye kufa hivi hapa kwa amani.