Swahili Hymn N-Z

Usinipite Mwokozi


Usinipite Mwokozi, unisikie;
Unapozuru wengine, usinipite.


Refrain
Yesu, Yesu, unisikie,
Unapozuru wengine, usinipite.


Kiti chako cha rehema, nakitazama
Magoti napiga pale, nisamehewe.


Sina ya kutegemea, ila wewe tu
Uso wako uwe kwangu, nakuabudu.


U mfariji peke yako, sina mbinguni
Wala duniani pote,Bwana mwingine.

https://youtu.be/sUWsB3YsHz8

 


Wachunga Walipolinda


Wachunga walipolinda
Kucha nyama zao,
Malaika mtukufu
Alishuka kwao.


Wakacha sana wachunga,
Akawatuliza,
‘Nawaletea habari
Ya kuwapendeza.‘


‘Mji ule wa Daudi
Leo amezawa
Mwokozi ni Kristo Bwana,
Ilivyoandikwa.‘


‘Huyo mwana wa Mbinguni
Ataonekana,
Amelazwa kihorini
Malazi hapana.‘


Alipokwisha yanena
Malaika hao
Waliimba wimbo huu
Usio na mwisho:


‘Enzi ni yake Mungu juu,
Na nchi salama,
Kwa watu nao radhi kuu,
Sasa na daima’.

 


Walio kifoni


1. Walio kifoni, nenda waponye,
Uwatoe walio shimoni;
Wanaoanguka uwainue;
Habari njema uwajulishe.


Ref
Walio kifoni waokoeni;
Mwokozi yuko huwangojea.


2. Wajapokawia anangojea,
Awasubiri waje tobani;
Mwokozi hawezi kuwadharau
Huwasamehe tangu zamani.


3. Na ndani ya moyo ya wanadamu,
Huwamo shida, tena huzuni;
Lakini kwa Yesu kuna rehema,
Kuwaponya na kuwaokoa.


4. Walio kifoni, nenda waponye;
Kazi ni yetu, zawadi iko;
Nguvu kuhubiri Bwana hutoa
Kwa subira tuwavute sasa.