Swahili Hymn N-Z

Nina haja Nawe


Nina haja nawe
Kila saa;
Hawezi mwingine
Kunifaa.


Refrain
Yesu nakuhitaji
Vivyo kila saa!
Niwezeshe Mwokozi,
Nakujia.


Nina haja nawe;
Kaa nami,
Na maonjo haya,
Hayaumi.


Nina haja nawe;
Kila hali,
Maisha ni bure,
Uli mbali.


Nina haja nawe;
Nifundishe
Na ahadi zako
Zifikishe.


Nina haja nawe;
Mweza yote,
Ni wako kabisa
Siku zote.

 


Ninao wimbo mzuri


1. Ninao wimbo mzuri, Tangu kuamini;
Wa Mkombozo Mfalme, Tangu kuamini.


Refrain:
Tangu kuamini, Tangu kuamini, Jina lake ‘tasifu,
Tangu kuamini, Nitalisifu jina lake.


2. Kristo anatosha kweli, Tangu kuamini,
Mapenzi yake napenda, Tangu kuamini.


3. Ninalo shuhuda sawa, Tangu kuamini,
Linalofukuza shaka, Tangu kuamini.


4. Ninalo kao tayari, Tangu kuamini,
Nililorithi kwa Yesu, Tangu kuamini.

 


Nipe Habari Za Yesu


1. Nipe habari za Yesu, Kwangu ni tamu sana:
Kisa chake cha thamani Hunipendeza sasa.
Jinsi malaika wengi walivyo imba sifa,
Alipoleta amani kwa watu wa dunia.


Ref
Nipe habari za Yesu, Kaza moyoni mwangu;
Kisa chake cha thamani Hunipendeza sana.


2. Kisa cha alivyofunga Peke yake jangwani.
Jinsi alivyomshinda Jaribu la Shetani;
Kazi aliyoifanya, Na siku za huzuni,
Jinsi walivyomtesa: Yote ni ya ajabu!


3. Habari za Msalaba Alivyosulubiwa;
Jinsi walivyo mzika, Akashinda kaburi.
Kisa chake cha rehema. Upendo wake kwangu.
Aliyetoa maisha Nipokee wokovu.