Wachunga Walipolinda
Wachunga walipolinda
Kucha nyama zao,
Malaika mtukufu
Alishuka kwao.
Wakacha sana wachunga,
Akawatuliza,
‘Nawaletea habari
Ya kuwapendeza.‘
‘Mji ule wa Daudi
Leo amezawa
Mwokozi ni Kristo Bwana,
Ilivyoandikwa.‘
‘Huyo mwana wa Mbinguni
Ataonekana,
Amelazwa kihorini
Malazi hapana.‘
Alipokwisha yanena
Malaika hao
Waliimba wimbo huu
Usio na mwisho:
‘Enzi ni yake Mungu juu,
Na nchi salama,
Kwa watu nao radhi kuu,
Sasa na daima’.
Waimba, Sikizeni
1. Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni;
Wimbo wa tamu sana, Wa pendo zake Bwana;
Duniani salama, Kwa wakosa rehema.”
Sisi sote na twimbe, Nao wale wajumbe;
Ref
Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni.
2. Ndiye Bwana wa mbingu, Tangu milele Mungu,
Amezaliwa mwili, Mwana wa mwanamwali;
Ametoka enzini, Kuja ulimwenguni
Mwokozi atufie, Ili tusipotee,
3. Seyidi wa amani, Ametoka Mbinguni,
Jua la haki, ndite, Atumulikiaye;
Amejivua enzi, Alivyo na mapenzi,
Ataka kutuponya, Kutuzalisha upya,
4. Njoo upesi, Bwana Twakutamani sana
Kaa nasi, Mwokosi Vita hatuviwezi
Vunja kichwa cha nyoka Sura zako andika
Tufanane na Wewe Kwetu sifa upewe.
Wakosaji fikirini
Wakosaji fikirini
Mwisho wa njia zenu!
Hamwogopi kupotezwa
Vibaya kuzimuni?
Rudini kwake Mwikozi!
Ref
Ndiye mwenye huruma,
Hawatupi wamjiao,
Njooni tu kwake Yesu!
Hapo mlipoyafuata
Mambo ya dunia hii,
Hamkuweza kuvivunja
Vifungo vya Shetani.
Rudini kwake Mwokozi.
Mambo yote hugeuka,
Tukimjua Mwokozi;
Twaondolewa makosa,
Tuwe wake Nwana tu.
Rudini kwake Mwokozi.