Swahili Hymn N-Z

Yesu Atupenda


Anipenda ni kweli
Mungu anena hili
Sisi wake watoto
Kutulinda si zito


Refrain
Yesu ni penda
Yesu ni penda
Yesu ni penda
Mungu amesema!

 


Yesu kwetu ni rafiki


Yesu kwetu ni Rafiki,
Huambiwa haja pia;
Tukiomba kwa Babaye
Maombi asikia;
Lakini twajikosesha,
Twajitweka vibaya;
Kwamba tulimwomba Mungu
Dua angesikia.


Una dhiki na maonjo?
Una mashaka pia?
Haifai kufa moyo,
Dua atasikia.
Hakuna mwingine mwema
Wakutuhurumia;
Atujua tu dhaifu;
Maombi asikia.


Je, hunayo hata nguvu,
Huwezi kwendelea,
Ujapodharauliwa
Ujaporushwa pia.
Watu wangekudharau
Wapendao dunia,
Hukwambata mikononi,
Dua atasikia.

 


Yesu nakupenda, U mali yangu


1. Yesu nakupenda, U mali yangu,
Anasa za dhambi sitaki kwangu;
Na Mwokozi aliyeniokoa,
Sasa nakupenda, kuzidi pia.


2. Moyo umejaa mapenzi tele
Kwa vile ulivyonipenda mbele,
Uhai wako ukanitolea
Sasa nakupenda, kuzidi pia.


3. Ulipoangikwa Msalabani
Tusamehewe tulio dhambini;
Taji ya miiba uliyoivaa,
Sasa nakupenda, kuzidi pia.


4. Niwapo hai, niwapo maiti,
Kupendana nawe kamwe siachi;
Hari za kifo zikinienea,
Sasa nakupenda, kuzidi pia.


5. Mawanda mazuri, na masikani
Niyatazamapo huko Mbinguni,
Tasema na taji nitakayovaa
Sasa nakupenda, kuzidi pia.