Swahili Hymn N-Z

Naendea msalaba


1. Naendea msalaba, Ni mnyonge, mpofu,
Yapitayo naacha nipe msalaba tu.


Ref
Nakutumaini tu, wee Mwana wa Mungu;
Nainamia kwako; Niponye sasa, Bwana.


2. Nakulilia sana: Nalemewa na dhambi;
Pole Yesu asema: “Nitazifuta zote.”


3. Natoa vyote kwako, nafasi nazo nguvu,
Roho yangu na mwili viwe vyako milele.


4. Kwa damu yake sasa amenivuta sana,
Upendo hubidisha, nimtafute Mwokozi.


5.Yesu yuaja tena! Nimepevuka kwake,
Kila chembe kamili; Msifuni yeye mponya!

 


Napenda Kuhubiri


1. Napenda kuhubiri habari ya Yesu,
Ya Bwana wa fahari na pendo zake kuu.
Huhubiri napenda kwa hali na mali;
Mwenyewe Nimeonja najua ni kweli.


Pambio
Napenda kuhubiri kisa cha Bwana Yesu,
Ya Bwana wa fahari na pendo Zake Kuu.


2. Napenda kuhubiri mambo ya ajabu
Na tukiyatafikiri yapita Dhahabu.
Kuhubiri napenda ya yaliyonifaa;
Nami sana napenda hayo kukwambia.


3. Napenda kuhubiri, hunifurahisha
Tamu yake habari haiwezi kwisha.
Napenda kuhubiri wa gizani nao;
hawana muhubiri wa kweleza chuo.


4. Kuhubiri napenda hata wajuao;
Kusikia hupenda kama wenzi wao.
Nako kwenye fahari nikiimba wimbo
Nitaimba habari ya Mwokozi huyo!

 


Nasifu Shani Ya Mungu


Nasifu shani ya Mungu, mweneza bahari,
Muumba pia wa mbingu, jua, nyota, mwezi,
Ni tukufu yako shani, mtengeza mambo,
Ya nyakati na zamani, yasiyo na mwisho.


Kadiri ya nionayo, ya kusifu Mungu;
Nchi niikanyagayo, na hayo mawingu;
Hakuna hata unyasi, usiokukuza;
Na upepo wavumisha, au kutuliza.


Nami kwa mkoni wako, naongozwa sawa,
Ni pato nikusifupo, kukwomba ni dawa;
Umenizingira nyuma, na mbele baraka;
Maarifa ya ajabu! Yanishinda mimi!

https://youtu.be/bd5M9ksUHns