Swahili Hymn N-Z

Neema ya Ajabu


1. Neema ya upendo wake
Neema kuu liko nami;
Kazi ya Yesu msalabani
Alipo mwaga damu yake.


Refrain
Neema yake, Neema, ya ajabu
Neema inayotakasa;
Neema yake, Neema, ya ajabu
Neema ishindayo dhambi.


2. Dhambi ni kama wimbi kubwa
Inayotishia maisha;
Ni neema isiyo kifani
Inayo ‘nyesha msalabani.


3. Neema hii ni ya ajabu
Iliyo bure kwetu sisi;
Wanaotaka kumuona
Watapata neema ya bure.

https://youtu.be/utm_Ot0p0ww


Neema ya pekee


Katika neema Nimeokolewa, Nilikuwa mimi Mnyonge
Nilikuwa kipofu bali neema ya Yesu, ilinifungua macho yangu


Nilikuwa mwenye hofu nilifungwa dhambini, nimefunguliwa sasa
Nitamsifu Bwana maishani mwote, kwani nina ushirika naye


Bwana ameniahidi mema, neno lake tumaini laokoa
Yeye atakuwa ngao yangu, siku zote maishani mwangu

 


Ni Heri Kifungo


Ni heri kifungo, Kinachotufunga
Mioyo yetu kwa pendo, Pendo la Kikristo


M-bele ya Baba Tunatoa sala;
Hofu, nia, masumbufu Yetu ni pamoja.


Tunavishiriki Matata na shida;
Na mara nyingi twatoa Chozi la fanaka.


Tunapoachana, Moyoni twalia;
Lakini tutakutana M-wisho mbinguni.

https://youtu.be/ZzR2n9weWq4