Swahili Hymn N-Z

Ogotera Kwa Nyasae


`Karar` as` embera, Yes` Omotoria;
Kaganya Koboka, Monen` one.


Refrain
Kaboka. korw` embera, Nobobui as` omobisa
Akabok` akabua omosunte
Amenyete n`abachenu kogamba
Kaboka, kaboka, Alleluy` akaboka.


Bakarend` embera, Yes` Omotoria;
Bakarenda bosa, Monen` one.


Tabuetwe nogokwa, Yes` Omotoria;
Kabu` ebisibo, Monen` one.

https://youtu.be/oad1CXWGcwA

 


Sayuni, ufrahi!


Sayuni, Ufurahi
Shangilia Yerusalemu!
Yuaja mfalme wako,
Mwenye amani kwako.
Sayuni, Ufurahi
Shangilia Yerusalemu!


Hosiana! Mesiya
Utubariki sasa
Jenga ufalme wako
Uimwenguni mwote.
Hosiana! Mesiya
Utubariki sasa


Hosiana! Pongezi!
Twaluamkia Bwana!
Kiti cha enzi yako
Chasimama milele.
Hosiana! Pongezi!
Twaluamkia Bwana!

 


Sijui Sababu Ya Neema


1. Sijui sababu ya neema
Niliyopewa na Mungu,
Sikulistahili pendo lake,
Wala wokovu wa Yesu;


Chorus
Namjua niliyemwamini,
Na kusadiki kwamba aweza
Kulinda kilichowekwa
Amana kwake Bwana.


2.Sijui jinsi nilivyopewa
Imani ya kumwamini,
Neno lake Yesu lilileta
Amani yake moyoni;


3.Sijui jinsi Roho wa Mungu
Awaonyeshavyo watu,
Wapate kuzitambua dhambi,
Na kumfuata Yesu.


4.Sijui kama mambo yajayo
Yatakuwa ya salama,
Lakini nitamwamini Yesu
Mpaka tutaonana.


5.Sijui siku gani ya Bwana
Hapa atakaporudi,
Nitamngojea na imani
Hata kumlaki hewani.