Swahili Hymn N-Z

Upendo wa Mungu Mkuu

 


Ushirika mkuu, furaha yangu


Ushirika mkuu, furaha yangu
Kumtegemea Bwana Yesu,
Nina baraka, amani pia,
Kumtegemea Bwana Yesu.


Chorus
Raha, Raha,
Nina raha na salama,
Raha, Raha,
Kwa kumtegemea Yesu.


Ni halisi kutembea naye,
Kwa kumtegemea Yesu.
Naona nuru njiani mwangu,
Kumtegemea Bwana Yesu.


Sioni shaka wala hasara,
Kumtegemea Bwana Yesu;
Nina amani kwake Mwokozi,
Kumtegemea Bwana Yesu.

 


Usiku Mtakatifu


Usiku mtakatifu, nyota zameremermeta
Ni usiku wa kuzawa mwokozi
Dunia yote, kwa dhambi ilizama
Hadi Yesu kaja kutuokoa
Tunaiingia ya kusisimua kote
Utukufu wake wachomoza
Tumsujudu, sikia malaika
Usiku mkuu, wa kuzaliwa Yesu Kristo
Usiku mkuu, usiku mtakatifu


Kweli ametufunza sote kupendana
Injili yake ni amani
Minyororo yote ya utumwa imevunjwa
Kwa jina lake tutapata uhuru
Tenzi tamu wa pamoja twainua
Tumsifu kwa roho zetu zote
Yesu ni Bwana, milele tumsifu
Tutangaze uweza na utukufu wake
Tutangaze uweza na utukufu wake