Yesu Atupenda
Anipenda ni kweli
Mungu anena hili
Sisi wake watoto
Kutulinda si zito
Refrain
Yesu ni penda
Yesu ni penda
Yesu ni penda
Mungu amesema!
Yesu Huita njooni kwangu
1. Yesu huita kwa upole mwingi, atwita wewe nami;
Moyoni mwetu hungoja, hukesha, Hukungojea wewe.
Ref
“Njoni kwangu, Mliochoka, njoni:
Yesu huita kwa upole mwingi, Akwita, “uje kwangu”
2. Atuombeapo usikawie, Hutuombea sisi;
Usidharau wema ma huruma, Huruma kwetu sisi.
3. Siku za maisha hupota hima, Hupita kwako, kwangu;
Usiku waja, kifo kinakuja, Huja kwako na kwangu.
4. Fikiri juu ya upendo wake, Upendo kwako, kwangu;
Dhambi zetu amekwisha samehe. Masamaha ni yetu.
Yesu kwetu ni rafiki
Yesu kwetu ni Rafiki,
Huambiwa haja pia;
Tukiomba kwa Babaye
Maombi asikia;
Lakini twajikosesha,
Twajitweka vibaya;
Kwamba tulimwomba Mungu
Dua angesikia.
Una dhiki na maonjo?
Una mashaka pia?
Haifai kufa moyo,
Dua atasikia.
Hakuna mwingine mwema
Wakutuhurumia;
Atujua tu dhaifu;
Maombi asikia.
Je, hunayo hata nguvu,
Huwezi kwendelea,
Ujapodharauliwa
Ujaporushwa pia.
Watu wangekudharau
Wapendao dunia,
Hukwambata mikononi,
Dua atasikia.