Swahili Hymn A-M

Mungu Wetu Ndiye Ngome


Mungu wetu ndiye ngome, silaha tena ngao.
Atukingiaye shida, zitushikazo sisi.
Adui wa kale, afanya hila,
Za kutushinda; ni mwenye nguvu kuu,
Hakuna amwezaye.


Nguvu zetu hazifai, tunashindwa upesi.
Lakini tunaye shujaa, aliye mwenye nguvu.
Jina lake nani? Ni Yesu Kristo;
Mungu mwenyewe; hapana mwingine,
Ni mshindaji wa wote.


Shetani akikusanya majeshi yake kote;
Hatuogopi kabisa, kwani tutawashinda.
Mfalme wa dunia, akunja uso;
Ana hasira, lakini ni bure,
Neno moja tu laweza.


Neno la mungu lashinda, halitafuti msaada.
Mungu yu pamoja nasi, na roho ya hekima.
Wakitunyang’anya watoto na wenzi;
Mwili nayo mali, haidhoru,si kitu;
Twamfuata Yesu mfalme.

 


Mwamba Wenye Imara


Mwamba wenye imara, kwako nitajificha
Maji hayo na damu, yaliyotoka humu
Hunisafi na dhambi, hunifanya Mshindi.


Kwa kazi zote pia, sitimizi sheria
Nijapofanya bidii, nikilia na kudhii
Hayaishi makosa, ndiwe wa kuokoa


Sina cha mkononi, naja msalabani
Nili tupu nivike, ni mnyonge nishike
Nili mchafu naja, Nioshe nisijafa.


Nikungojapo chini, na kwenda kaburini
Nipaapo mbinguni, na kukuona enzini
Roho yangu na iwe, rahani mwako wewe.

or


Mwamba wenye imara,
Kwako nitajificha,
Maji hayo na damu,
Yaliyotoka humu,
Hunisafi na dhambi,
Hunifanya mshindi.


Kwa kazi zote pia,
Sitimizi sheria,
Nijapofanya bidii,
Nikilia na kudhii,
Hayaishi makosa,
Ndiwe wa kuokoa.


Sina cha mkononi,
Naja msalabani,
nili tupu, Nivike,
Ni mnyonge, nishike,
Nili mchafu naja,
Nioshe nisijafa.


Nikungojapo chini,
Na kwenda kaburini,
Nipaapo mbinguni,
Na kukwona enzini,
Roho yangu na iwe,
Rahani mwako wewe.

 


Mwokozi ajabu ni Yesu bwana

 


Mwokozi kama mchunga


Mwokozi kama mchunga
Utuongoze leo;
Ututume malishoni;
Fanya tayari boma.
Bwana Yesu, peke yako
Umetuvuta kwako.


Tu wako, uwe rafiki,
Uwe mlinzi wetu;
Kundi lako ulilinde,
Tusivutwe na dhambi;
Bwana Yesu tusikie,
Tukiomba, samehe.


Umetuahidi kwamba
Utakubali watu,
Utawahurumia na
Utawapa neema;
Bwana Yesu, tunapenda
Kuwa wako.