Swahili Hymn A-M

Ee Mungu Msaada Wa Zamani


Ee Mungu Msaada Wa Zamani
Na tumaini letu
Makimbilio taabuni
Makao ya milele.


Kwa mkono wangu ulilinda
Watakatifu wako
Pasipo hofu walikaa
Wakikutegemea.


Zamani sana ulimwengu
Haujaumbwa bado
Tokea mwanzo ndiwe Mungu
U Mungu wa milele.


Miaka elfu mbele zako
Ni kama siku moja
Ni kama kesha la usiku
Kunapopambazuka.


Upesi siku zinapita
Huenda zao wote
Huenda zao kama ndoto
Haikumbukwi mchana.


Ee Mungu msaada Wa Zamani
U tumaini letu
Utuhifadhi taabuni
Na leo na milele.

 


Eneza Habari Humu Duniani


Eneza Habari Humu Duniani
Po pote panapo moyo wa huzuni;
Ndimi za Wakristo zitangaze Neno,
Yopo Mfariji.


Ref
Yopo Mfariji, Yopo Mfariji
Roho Mtakatifu, ndiye Msaidizi;
Eneza Habari Humu Duniani,
Yopo Mfariji.


Mfalme wa wafalme, Yesu, umtazame,
Amectuletea siha ya milele;
Mateka wapate Ukombozi wake,
Yopo Mfariji.


Niwezeje mimi kutamka vizuri,
Kumsifu Mwokozi aliye mbinguni?
Nitangaze sasa, neno la furaha,
Yopo Mfariji.


Wenzangu, tuimbe nyimbo za milele,
Mbinguni tujaze na shukrani teLe;
Upendo wa Bwana ujulike sana,
Yopo Mfariji.

 


Fikira Moja Tu


Fikira moja tu Hurejea tena
Nimekaribia mbingu Zaidi ya jana.


Shika
Karibu na kwetu mbinguni,
Karibu na kwetu sasa,
Nikuone karibu.


Karibu na kwetu Na kwenye makao
Kiti cha enzi cha Mungu, pahali pa mto.


Kamilisha, Yesu, Kuamini kwangu
Nikifika mwisho wangu, Nikuone karibu.

https://youtu.be/5pSgMyac2Ug

 


Furaha kwa ulimwengu


Furaha kwa ulimwengu, Bwana atakuja!
Kila moyo umpokee,
Viumbe imbeni,Viumbe imbeni, Viumbe vyote Imbeni.
Viumbe imbeni,Viumbe imbeni, Viumbe vyote Imbeni.


Na Bwana atatawala: Watu na waimbe;
Mit, milima na mawe
Kariri furaha, Kariri furaha, Kariri furaha kubwa.
Kariri furaha, Kariri furaha, Kariri furaha kubwa.


Atatawala kwa wema; Atawafundisha
Mataifa haki yake,
Ajabu za pendo,Ajabu za pendo, Ajabu za pendo lake.
Ajabu za pendo,Ajabu za pendo, Ajabu za pendo lake.