Swahili Hymn A-M

Msalabani Pa mwokozi


1.Msalabani pa mwokozi,
Hapo niliomba upozi,
Akaniokoa mpenzi,
Mwana wa Mungu.


Ref
Mwana wa Mungu,
Mwokozi wangu,
Akaniokoa mpenzi,
Mwana wa Mungu.


2.Chini ya mti msumbufu,
Niliomba utakatifu,
Alinikomboa kwa damu,
Mwana wa Mungu.


3.Aliniokoa dhambini,
Ikawa kunikaa ndani,
Aliponifia mtini,
Mwana wa Mungu.


4.Damu ya Yesu ya thamani,
Huniokoa makosani,
Huniendesha wokovuni,
Mwana wa Mungu.


5.Hicho kijito cha gharama,
Leo jivike kwa kuzama,
Kwake uuone uzima,
Mwana wa Mungu.

 


Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu


1. U Mtakatifu! Mungu Mwenyezi!
Alfajiri Sifa Zako Tutaimba;
U Mtakatifu, Bwana Wa Huruma.
Mungu Wa vyote Hata Milele.


2. U Mtakatifu! Na Malaika
Wengi Sana WanaKuabudu Wote;
Elfu Na Maelfu WanaKusujudu
Wa zamani Na Hata Milele.


3. U Mtakatifu! Ingawa Giza
Lakuficha Fahari Tusiioone,
U Mtakatifu! Wewe Peke Yako,
Kamili Kwa Uwezo Na Pendo.

 


Mungu atukuzwe


1. Mungu atukuzwe, kwa mambo makuu,
Upendo wake ulitupa yesu,
Aliyejitoa maisha yake,
Tuwe nao uzima wa milele.


Refrain
Msifu, msifu dunia sikia;
Msifu, msifu, watuwafurahi;
Na uje kwa baba, kwa yesu mwana
Ukamtukuze kwa mambo yote.


2. Wokovu kamili zawadi kwetu,
Ahadi ya mungu kwa ulimwengu;
Wanaomwamini na kuungama,
Mara moja wele husamehewa.


3. Alitufundisha mambo makuu,
Alihakikisha wokovu wetu;
Lakini zaidi ajabu kubwa,
Yesu atakuja na tutamwona.