Swahili Hymn A-M

Mbali kule nasikia


Mbali kule nasikia malaika wa mbinguni,
Wakiimba wengi pia wimbo huo juu angani:


Ref
Gloria in excelsis Deo,
Gloria in excelsis Deo.


Wachunga tuambieni sababu ya nyimbo hizo?
Mwenye kuimbiwa ni nani, juu ya nani sifa hizo?


Je hamjui jambo kuu la kuzaliwa Mwokozi?
Habari ya wimbo huo ndiyo kumshukuru Mwenyezi.


Kweli, nasi twende hima, tufike kule aliko,
Tuone mtoto na mama, tuwasalimie huko.

 


Mbele Ninaendelea


ninaendelea ninazidi kutembea
maombi uyasikie eeh bwana unupandishe,


Refrain
Ee bwana uniinue kwa imani nisimame
nipande milima yote Ee bwana unipandishe,


Nataka nipandishwe juu zaidi yale mawingu
nitaomba nifikishwe ee bwana unipandishe,


Sina tamaani nikae mahali pa shaka kamwe
hapo wengi wanakaa kuendelea naomba,


Nisikae duniani ni mahali pa shetani
natazamia mbinguni nitafika kwa imani,

 


Msalaba ndio Asili ya Mema


Sioni haya kwa Bwana,
Kwake nitang’ara!
Mti wake sitakana,
Ni neno imara.


Ref
Msalaba ndio asili ya mema,
Nikatua mzigo hapo;
Nina uzima, furaha daima,
Njoni kafurahini papo.


Kama kiti chake vivyo,
Ni yake ahadi;
Alivyowekewa navyo,
Kamwe, havirudi.


Bwana wangu, tena Mungu,
Ndilo lake jina!
Hataacha roho yangu,
Wala kunikana.


Atakiri langu jina,
Mbele za Babaye,
Anipe pahali tena,
Mbinguni nikae.