Swahili Hymn A-M

Bwana Amefufuka Haleluya


1. Bwana amefufuka, Aleluya.
Twimbe na malaika, Aleluya.
Sifa zetu na shangwe, Aleluya.
Na zao zisitengwe, Aleluya.


2. Ukombozi timamu, Aleluya.
Umetimu kwa damu, Aleluya.
Mshindi asifiwe, Aleluya.
Yu hai kwa milele. Aleluya.


3. Jiwe, lindo, muhuri, Aleluya.
Vi wapi? Na kaburi? Aleluya.
Kifo hakimuweki, Aleluya.
Ametoka peponi, Aleluya.


4. Yu hai mtukufu; Aleluya.
Cha kifo hatuhofu! Aleluya.
Alitufia sisi, Aleluya.
Tuwe mahuru nasi, Aleluya.


5. Kichwa chatangulia, Aleluya.
Tupae, nasi, pia!, Aleluya.
Kwa kuwa tuna fungu, Aleluya.
Mti, kaburi, mbinguni, Aleluya.


6. Ndiwe Mwokozi wetu, Aleluya.
Sifa ni yako Yesu, Aleluya.
Utukuzwe pekeo, Aleluya.
Ni wewe ufufuo, Aleluya.

 


Bwana nasikia kwamba


1. Bwana nasikia kwamba
umebariki wengi,
nami nakuomba sasa:
Nibariki na mimi!


Chorus
Na mimi na mimi
Nibariki na mimi.


2. Nipitie Baba yangu,
kweli mimi mkosaji,
Baba uingie kwangu,
nirehemu na mimi!


3. Nipitie, nakuomba,
Bwana Yesu, Mwokozi,
wakosaji wawaita,
uniite na mimi!


4. Nipitie Roho mwema
kweli mimi sioni,
mwenye nguvu za kuponya,
nipe nguvu na mimi!


5. Nipitie Baba yangu,
nakuomba kwa bidii,
umebariki wengine,
nibariki na mimi!

 


Bwana upepo wavuma


Bwana upepo wavuma! Wimbi lina ghadhabu! Wingu hili linanguruma bandari si karibu,
Hali yetu hufikiri kwa nini kulala? Twafa maji yawe ni karibu wokovu la! Hapana


Refrain
Pepo na mawimbi vyasikia tulia, tulia, kama ukali wa bahari, wanadamu, pepo na shetani
Mawimbi yapataje kuumiza chombo kilicho na Yesu Bwana?
Mambo pia viamsikia tulia, tulia Mambo pia viamsikia tulia, tulia


Bwana nimezima moyo hamu yanizidi tu ninasumbuka roho yangu uniokoe Bwana;
Dhambi nyingi na uovu zitanizamisha Bwana wangu upesi ni wewe utakaenitosha,


Sasa hofu imekwisha ni shwari baharini, Jua letu tena linang’ara utulivu rohoni
Kaa nami ewe Bwana nisiwe mimi tu nami nitafika bandarini ng’ambo niko nafuu