Anaishi
Mwana wa Mungu Jina ni Yesu
Alikufa, Tuokoke
Deni langu, Akalilipa
Amefufuka, mwokozi anaishi
Pambio
Anaishi, mimi sina shaka
Anaishi, siogopi
Mimi najua anayo kesho
Maisha bora, maana yeye anaishi.
Yapendeza kuwa na mwana
Ni furaha anakupa
Kwani ipo hipo dhamana
Kuona kesho, maana yeye anaishi
Siku moja, nitavuka mto
Vito vyangu vikomapo
Nikishinda hayo mauti
Nitaingia utukufuni, atawala
Anisikiaye Aliye Yote
1. Anisikiaye, awaye yote;
Sasa litangaze, wajue wote,
Duniani kote neno wapate,
Atakaye na aje!
Chorus
Ni “Atakaye”, ni “atakaye”,
Pwani hata bara, nalitangazwe;
Ni Baba Mpenzi awaitaye,
Atakaye na aje.
2. Anayenijia, Yesu asema,
Na Asikawie, aje mapema,
Mimi ndimi njia, kweli, uzima;
Atakaye na aje!
3. Atakaye aje, ndiyo ahadi;
Atakaye, kweli ni ya, milele,
Atakaye hilo wote wapate,
Atakaye na aje.
Baada Ya Kazi na tabu zote
Baada ya kazi na taabu zote
Nikiingia kwenye furaha,
Kumwona Yesu, Kumwabudia,
Kutakuwa furaha yangu kuu.
Ref
Kumwona tu ni furaha,
Kumwona tu ni furaha
Nikiondolewa shida zote,
Nikiona uso wa Bwanangu.
Mwenye rehema anipendaye,
Akinipa Kikao mbinguni.
Nitamfurahia mponya wangu,
Kwa kumwona tu uso kwa uso.
Pale mbinguni kwenye furaha,
Nitaonana na ndugu wengi
Lakini kumwona Bwana Yesu,
Kutakuwa furaha kabisa.
Baba Yetu Aliye Mbinguni
Baba yetu aliye mbinguni, Amenifurahisha yakini;
Kuniambia mwake Chuoni, Ya kuwa nami Yesu pendoni.
Refrain:
Anipenda Mwokozi Yesu, Anipenda, Anipenda:
Anipenda, Mwokozi Yesu, Anipenda mimi.
Nimuachapo kutanga mbali, Yeye yu vivyo, hupenda kweli:
Hunirejeza kwake moyoni, Kweli yu nami Yesu pendoni.
Anipenda! Nami ninampenda, Kwa wokovu alionitenda;
Akanifilia Msalabani, Kwa kuwa nami Yesu pendoni.
Bwana Amefufuka Haleluya
1. Bwana amefufuka, Aleluya.
Twimbe na malaika, Aleluya.
Sifa zetu na shangwe, Aleluya.
Na zao zisitengwe, Aleluya.
2. Ukombozi timamu, Aleluya.
Umetimu kwa damu, Aleluya.
Mshindi asifiwe, Aleluya.
Yu hai kwa milele. Aleluya.
3. Jiwe, lindo, muhuri, Aleluya.
Vi wapi? Na kaburi? Aleluya.
Kifo hakimuweki, Aleluya.
Ametoka peponi, Aleluya.
4. Yu hai mtukufu; Aleluya.
Cha kifo hatuhofu! Aleluya.
Alitufia sisi, Aleluya.
Tuwe mahuru nasi, Aleluya.
5. Kichwa chatangulia, Aleluya.
Tupae, nasi, pia!, Aleluya.
Kwa kuwa tuna fungu, Aleluya.
Mti, kaburi, mbinguni, Aleluya.
6. Ndiwe Mwokozi wetu, Aleluya.
Sifa ni yako Yesu, Aleluya.
Utukuzwe pekeo, Aleluya.
Ni wewe ufufuo, Aleluya.