Lo Ajabu Kupata Uzima
Lo! Ajabu kupata Uzima, katika damu ya Mwokozi wangu!
Alinifilia pendoni, Mimi niliyemsulubisha!
Upendo huu wa kushangaza kabisa Wewe Kristo wangu kunifilia pendoni
Upendo huu nashangaa Kristo wangu kunifilia
wangu alitoa damu Siwezi kuelewa neno hili,
Viumbe vyote vya mbinguni Navyo haviwezi kufahamu
Najua tu ni kwa rehema zake Mungu Malaika wote wamsujudu Mungu
Ni rehema tumwabudu, Tumwamini ndiye mwokozi
Aliondoka kule mbinguni Kwa nyumba yake Mungu Baba yake
Na utukufu aliacha Afe kwa ajili ya waovu
Rehema zake ni nyingi na ukarimu Kwani Mungu wangu aliniokoa mimi
Sistahili neema yake, Lakini aliniokoa
Roho yangu ilifungwa sana Dhambi na giza vilinilemea
Ukaniangaza rohoni, Gereza yangu ikaang’aa mno
Ikafunguka minyororo yangu yote Nikaondoka nikaanza kukufuata
Siku ile nitapata Uhuru kweli kwako Mungu
Hukumuni mimi simo sasa Mimi ni wake Yesu ndiye wangu
Yeye ni kichwa changu kweli Na amenivika haki yake
Mimi hodari sasa kwa kiti cha Enzi Napewa taji ya milele katika Yesu
Sina hofu kusogea Katika Bwana wangu Kristo
Malaika kaleta noeli
Malaika kaleta Noeli ya kwanza,
Kwa wachunga kondoo katika makonde,
Bethlehemu wakawa walinzi wa zamu,
Wakaona usiku ajabu ya nuru
Refrain
Noeli, Noeli, Noeli, Noeli,
Yesu yu Mungu na binadamu
Noeli, Noeli, Noeli, Noeli,
Yesu yu Mungu na binadamu
Wakaona mbinguni, mwangaza wa nyota,
Ing’aayo kwa mbali na masharikini,
Wakaenda upesi, walivyoambiwa.
Bethlehemu wamwone Mwokozi horini
Mashariki watoka wafalme watatu,
Mamajusi waliotafuta mfalme,
Wafuata hii nyota waliyoiona,
Wasipate kumkosa wanayemtafuta
Kiongozi ni nyota iliyowaleta
Hata mji wa Daudi alimozaliwa
Ikakaa mara moja isiendelee
Pale pale nyumbani alimo Mwokozi
Mamajusi walipoingia nyumbani
Wakapiga magoti kwa heshima kuu
Mara hiyo walipozifungua hazina
Manemane, uvumba, dhahabu, watoa
Mapenzi yako yafanyike
Mapenzi yako yafanyike,
Wewe mfinyanzi, nami towe,
Unifinyange upendavyo,
Mimi tayari, naja kwako.
Mapenzi yako yafanyike,
Unihoji dhambi zote,
Unisafishe vya kimwili,
Niinamapo Msalabani.
Mapenzi yako yafanyike,
Mimi dhaifu, mimi mnyonge.
Uwezo wote, kwako kweli,
Sasa niponye, Ee, Mwokozi.
Mapenzi yako yafanyike,
Natoa kwako vitu vyote,
Maisha, mali, moyo, mwili,
Vyote ni vyako, kweli, kweli.
Mapenzi yako yafanyike,
Mapenzi yangu yavunjike,
Ninakubali uwe Bwana,
Ni mali yako, twaa kabisa.
Mapenzi yako yafanyike,
Unitawale siku zote,
Sura ya Yesu umba kwangu,
Nijaze Roho nayo nguvu.