Swahili Hymn N-Z

Yesu ni Jina Nipendalo


Yesu ni jina nipendalo. Napenda kulisikia;
Napenda kulitamka hilo, Lililoniridhisha.


Chorus
Yesu, nakupenda, Yesu, nakupenda;
Yesu, naktipenda, Kwani ulinipenda.


Jina hilo huniambia, Mwokozi alinipenda;v Damu yake ilimwagika, Nipate kuokoka.


Lanionyesha sifa yake, Iliyo katika Baba;
Njia ijapokuwa giza, Yesu huniongoza.


Lanidhihirishia Yesu, Aliyenihurumia;
Laondoa taabu yangu, Niwe wake daima.

 


Yote namtolea Yesu


Yote namtolea Yesu, Nampa moyo wote,
Nitampenda siku zote, Namwandama kila saa.


Chorus
Yote kwa Yesu,Yote kwa Yesu,
Yote kwako, Ee Mwokozi, Natoa sasa.


Yote namtolea Yesu, Nainamia pake;
Nimeacha na anasa, Kwako Yesu nipokee,


Yote namtolea Yesu, Nifanye niwe wako;
Nipe Roho yako, Bwana, Anilinde daima,


Yote namtolea Yesu, Nami naona sasa;
Furaha ya ukombozi, Nasifu jina lake.