Swahili Hymn N-Z

Unahitaji Uhuru Kweli


Unahitaji Uhuru Kweli? Mwamini Yesu, Mwamini Yesu,
Ana uwczo kukukomboa, Sasa umwamini Yesu.


Ref
Bwana Yesu ana uwezo, Uwezo kwa damu;
Bwana Yesu ana uwezo, Kukuokoa Kweli.


Unahitaji kutakasika? Mwamini Yesu, Mwamini Yesu,
Utasafishwa kwa Roho wake, Sasa umwamini Yesu.


Uwe mwenye moyo safi mno, Uko uwezo wa ajabu;
Alama itoke kwa uwezo, Damuni mwa Mwana Yesu.


Ufanye kazi kwa Mfalme Yesu, Uko uwezo wa ajabu;
Uishi daima kumsifu, Damuni mwa Mwana Yesu.

 


Upendo wa Mungu Mkuu

 


Ushirika mkuu, furaha yangu


Ushirika mkuu, furaha yangu
Kumtegemea Bwana Yesu,
Nina baraka, amani pia,
Kumtegemea Bwana Yesu.


Chorus
Raha, Raha,
Nina raha na salama,
Raha, Raha,
Kwa kumtegemea Yesu.


Ni halisi kutembea naye,
Kwa kumtegemea Yesu.
Naona nuru njiani mwangu,
Kumtegemea Bwana Yesu.


Sioni shaka wala hasara,
Kumtegemea Bwana Yesu;
Nina amani kwake Mwokozi,
Kumtegemea Bwana Yesu.