Swahili Hymn N-Z

Twendeni askari


1. Twendeni askari, watu wa Mungu,
Yesu yuko mbele, tumwandame juu,
Ametangulia Bwana Vitani,
Twende mbele kwani ndiye amini.


Ref
Twendeni askari, watu wa Mungu,
Yesu yuko mbele, tumwandame juu


2. Jeshi la shetani, Likisikia
Jina la Mwokozi, Litakimbia
Kelele za shangwe, Zivume nchini;
Ndugu inueni zenu sauti.


3. Kweli kundi ndogo, watu wa Mungu,
Sisi Na Mababa tu moja fungu,
Hatutengwi nao, moja imani, Tumaini
moja, na moja dini.


4. Haya mbele watu Nasi njiani,
Inueni nyoyo, Nanyi sifuni;
Heshima na sifa ni ya Mfalme,
Juu hata chini, sana zivume.

 


Uliniimbie tena, Neno la Uzima


Uliniimbie tena, Neno la uzima
Uzuri wake nione, Neno la uzima
Neno hili zuri, lafundisha kweli


Ref
Maneno ya uzima ni maneno mazuri
Manemo ya uzima ni naneno mazuri


Kristo anatupa sote, Neno la uzima
Mwenye dhambi asikie Neno la uzima
Latolewa bure, Tupate wokovu


Neno tamu la Injili, neno la uzima
Mwenye dhambi asikie Neno la uzima
Litatutakasa, kwa haki ya Mwana

 


Umechoka Umesumbuka


Umechoka, je, umesumbuka? mwambie Yesu sumbuko lako;
Unayalilia yapitayo? mwambie Yesu pekee.


Refrain
Mwambie Yesu sumbuko lako, yu rafiki amini,
Hakuna rafiki kama yeye, mwambie Yesu pekee.


Je, machozi yakulengalenga? mwambie Yesu sumbuko lako;
Walemewa na dhambi rohoni? mwambie Yesu pekee.


Waogopa shida na majonzi? mwambie Yesu sumbuko lako;
Wasumbukia mambo yajayo? mwambie Yesu pekee.


Kuanzia kifo kukutisha? mwambie Yesu sumbuko lako;
Watamania ufalme wake? mwambie Yesu pekee.

https://youtu.be/v3ACbLT04KU