Twamsifu Mungu
1. Twamsifu Mungu kwa Mwana wa pendo
Aliyetufia na kupaa juu.
Refrain:
Aleluya! Usifiwe; Aleluya! Amin.
Aleluya! Usifiwe; utubariki.
2. Twamsifu Mungu kwa Roho Mtukufu,
Ametufunula Mwokozi wetu.
3. Twamsifu Mwana, aliyetufia,
Aliyetwaa dhambi akazifuta.
4. Twamsifu Mungu wa neema yoge,
Ametukomboa akatuongoza.
5. Tuamshe tena, tujaze na pendo,
Na moyoni uwashe moto wa Roho.
Twapanda Mapema
Twapanda mapema, na mchana kutwa
Mbegu za fadhili hata jioni;
Twangojea sasa siku za kuvuna:
Tutashangilia wenye mavuno.
Refrain
Wenye mavuno, wenye mavuno,
Tutashangilia wenye mavuno.
Wenye mavuno, wenye mavuno,
Tutashangilia Wenye mavuno.
Twapanda mwangani na kwenye kivuli;
Tusishindwe na baridi na pepo;
Punde itakwisha kazi yetu hapa:
Tutashangilia wenye mavuno.
Twapanda kwa Bwana mbegu kila siku,
Tujapoona taabu na huzuni;
Tuishapo shinda atatupokea:
Tutashangilia wenye mavuno.
Twende Kwa Yesu
1.Twende kwa Yesu mimi nawe, njia atuonya tuijue,
Imo chuoni; na mwenyewe, hapa asema njoo!
Ref
Na furaha tutaiona, myoyo iki takasa sana;
Kwako mwokozi, kuonana, na milele kukaa.
2. “Wana na waje,” atwambia furahini kwa kusikia;
Ndiye Mwokozi wetu hasa, na tumtii, njoni.
3. Wangojeani? Leo yupo: sakiza sana asemapo;
Huruma zake zitwitapo, ewe kijana, njoo.
https://youtu.be/fdRhiwlVpuo
Twende Kwa Yesu
1.Twende kwa Yesu mimi nawe, njia atuonya tuijue,
Imo chuoni; na mwenyewe, hapa asema njoo!
Ref
Na furaha tutaiona, myoyo iki takasa sana;
Kwako mwokozi, kuonana, na milele kukaa.
2. “Wana na waje,” atwambia furahini kwa kusikia;
Ndiye Mwokozi wetu hasa, na tumtii, njoni.
3. Wangojeani? Leo yupo: sakiza sana asemapo;
Huruma zake zitwitapo, ewe kijana, njoo.
https://youtu.be/fdRhiwlVpuo