Swahili Hymn N-Z

Twapanda Mapema


Twapanda mapema, na mchana kutwa
Mbegu za fadhili hata jioni;
Twangojea sasa siku za kuvuna:
Tutashangilia wenye mavuno.


Refrain
Wenye mavuno, wenye mavuno,
Tutashangilia wenye mavuno.
Wenye mavuno, wenye mavuno,
Tutashangilia Wenye mavuno.


Twapanda mwangani na kwenye kivuli;
Tusishindwe na baridi na pepo;
Punde itakwisha kazi yetu hapa:
Tutashangilia wenye mavuno.


Twapanda kwa Bwana mbegu kila siku,
Tujapoona taabu na huzuni;
Tuishapo shinda atatupokea:
Tutashangilia wenye mavuno.

 


Twende Kwa Yesu


1.Twende kwa Yesu mimi nawe, njia atuonya tuijue,
Imo chuoni; na mwenyewe, hapa asema njoo!


Ref
Na furaha tutaiona, myoyo iki takasa sana;
Kwako mwokozi, kuonana, na milele kukaa.


2. “Wana na waje,” atwambia furahini kwa kusikia;
Ndiye Mwokozi wetu hasa, na tumtii, njoni.


3. Wangojeani? Leo yupo: sakiza sana asemapo;
Huruma zake zitwitapo, ewe kijana, njoo.

https://youtu.be/fdRhiwlVpuo

 


Twende Kwa Yesu


1.Twende kwa Yesu mimi nawe, njia atuonya tuijue,
Imo chuoni; na mwenyewe, hapa asema njoo!


Ref
Na furaha tutaiona, myoyo iki takasa sana;
Kwako mwokozi, kuonana, na milele kukaa.


2. “Wana na waje,” atwambia furahini kwa kusikia;
Ndiye Mwokozi wetu hasa, na tumtii, njoni.


3. Wangojeani? Leo yupo: sakiza sana asemapo;
Huruma zake zitwitapo, ewe kijana, njoo.

https://youtu.be/fdRhiwlVpuo