Bwana nasikia kwamba
1. Bwana nasikia kwamba
umebariki wengi,
nami nakuomba sasa:
Nibariki na mimi!
Chorus
Na mimi na mimi
Nibariki na mimi.
2. Nipitie Baba yangu,
kweli mimi mkosaji,
Baba uingie kwangu,
nirehemu na mimi!
3. Nipitie, nakuomba,
Bwana Yesu, Mwokozi,
wakosaji wawaita,
uniite na mimi!
4. Nipitie Roho mwema
kweli mimi sioni,
mwenye nguvu za kuponya,
nipe nguvu na mimi!
5. Nipitie Baba yangu,
nakuomba kwa bidii,
umebariki wengine,
nibariki na mimi!
Bwana upepo wavuma
Bwana upepo wavuma! Wimbi lina ghadhabu! Wingu hili linanguruma bandari si karibu,
Hali yetu hufikiri kwa nini kulala? Twafa maji yawe ni karibu wokovu la! Hapana
Refrain
Pepo na mawimbi vyasikia tulia, tulia, kama ukali wa bahari, wanadamu, pepo na shetani
Mawimbi yapataje kuumiza chombo kilicho na Yesu Bwana?
Mambo pia viamsikia tulia, tulia Mambo pia viamsikia tulia, tulia
Bwana nimezima moyo hamu yanizidi tu ninasumbuka roho yangu uniokoe Bwana;
Dhambi nyingi na uovu zitanizamisha Bwana wangu upesi ni wewe utakaenitosha,
Sasa hofu imekwisha ni shwari baharini, Jua letu tena linang’ara utulivu rohoni
Kaa nami ewe Bwana nisiwe mimi tu nami nitafika bandarini ng’ambo niko nafuu
Chakutumaini sina
1. Cha kutumaini sina,
Ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha,
Dhambi zangu kuziosha.
Ref
Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama.
2. Njia yangu iwe ndefu,
Yeye hunipa wokovu,
Mawimbi yakinipiga,
Nguvu ndizo nanga.
3. Damu yake na sadaka,
Nategemea daima,
Yote chini yakiisha,
Mwokozi atanitosha.
4. Njia yangu iwe ndefu,
Yeye hunipa wokovu
Mawimbi yakinipiga,
nguvu zake ndiyo nanga