Mungu atukuzwe
1. Mungu atukuzwe, kwa mambo makuu,
Upendo wake ulitupa yesu,
Aliyejitoa maisha yake,
Tuwe nao uzima wa milele.
Refrain
Msifu, msifu dunia sikia;
Msifu, msifu, watuwafurahi;
Na uje kwa baba, kwa yesu mwana
Ukamtukuze kwa mambo yote.
2. Wokovu kamili zawadi kwetu,
Ahadi ya mungu kwa ulimwengu;
Wanaomwamini na kuungama,
Mara moja wele husamehewa.
3. Alitufundisha mambo makuu,
Alihakikisha wokovu wetu;
Lakini zaidi ajabu kubwa,
Yesu atakuja na tutamwona.
Mungu Wetu Ndiye Ngome
Mungu wetu ndiye ngome, silaha tena ngao.
Atukingiaye shida, zitushikazo sisi.
Adui wa kale, afanya hila,
Za kutushinda; ni mwenye nguvu kuu,
Hakuna amwezaye.
Nguvu zetu hazifai, tunashindwa upesi.
Lakini tunaye shujaa, aliye mwenye nguvu.
Jina lake nani? Ni Yesu Kristo;
Mungu mwenyewe; hapana mwingine,
Ni mshindaji wa wote.
Shetani akikusanya majeshi yake kote;
Hatuogopi kabisa, kwani tutawashinda.
Mfalme wa dunia, akunja uso;
Ana hasira, lakini ni bure,
Neno moja tu laweza.
Neno la mungu lashinda, halitafuti msaada.
Mungu yu pamoja nasi, na roho ya hekima.
Wakitunyang’anya watoto na wenzi;
Mwili nayo mali, haidhoru,si kitu;
Twamfuata Yesu mfalme.
Mwamba Wenye Imara
Mwamba wenye imara, kwako nitajificha
Maji hayo na damu, yaliyotoka humu
Hunisafi na dhambi, hunifanya Mshindi.
Kwa kazi zote pia, sitimizi sheria
Nijapofanya bidii, nikilia na kudhii
Hayaishi makosa, ndiwe wa kuokoa
Sina cha mkononi, naja msalabani
Nili tupu nivike, ni mnyonge nishike
Nili mchafu naja, Nioshe nisijafa.
Nikungojapo chini, na kwenda kaburini
Nipaapo mbinguni, na kukuona enzini
Roho yangu na iwe, rahani mwako wewe.
or
Mwamba wenye imara,
Kwako nitajificha,
Maji hayo na damu,
Yaliyotoka humu,
Hunisafi na dhambi,
Hunifanya mshindi.
Kwa kazi zote pia,
Sitimizi sheria,
Nijapofanya bidii,
Nikilia na kudhii,
Hayaishi makosa,
Ndiwe wa kuokoa.
Sina cha mkononi,
Naja msalabani,
nili tupu, Nivike,
Ni mnyonge, nishike,
Nili mchafu naja,
Nioshe nisijafa.
Nikungojapo chini,
Na kwenda kaburini,
Nipaapo mbinguni,
Na kukwona enzini,
Roho yangu na iwe,
Rahani mwako wewe.