Japo Dhambi Ni Nyekundu
1. Japo dhambi ni nyekundu,
Zitakuwa nyeupe,
Japo dhambi ni nyekundu,
Zitakuwa nyeupe,
Japo kuwa ni nyekundu
Takuwa safi
Japo dhambi ni nyekundu,
Japo dhambi ni nyekundu,
Zitakuwa nyeupe,
Zitakuwa nyeupe.
2. Sikia sauti yake
Umurudie Mungu
Sikia sauti yake
Umurudie Mungu
Mungu yeye wa huruma,
Mwenye upendo
Sikia sauti yake
Sikia sauti yake
Umurudie Mungu
Umurudie Mungu
3. Utasamehewa dhambi
Na hatazikumbuka,
Utasamehewa dhambi
Na hatazikumbuka,
Asema tumutazame
Yeye asema
Utasamehewa dhambi
Utasamehewa dhambi
Na hatazikumbuka,
Na hatazikumbuka.
https://www.youtube.com/watch?v=B3m9WDq4p24
Jina la Yesu Salamu(Diadem)
1. Jina la Yesu, salumu!
Lisujudieni, Lisujudieni;
Ninyi mbinguni, hukumu,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.
2. Enzi na apewa kwenu,
Wateteea dini, Watetea dini;
Mkuzeni Bwana wenu
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.
3. Enyi mbegu ya rehema,
Nanyi msifuni, Nanyi msifuni;
Mmeponywa kwa neema,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.
4. Wenye dhambi kumbukeni,
Ya msalabani, Ya msalabani,
Kwa furaha msifuni,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.
5. Kila mtu duniani
Msujudieni, Msujudieni;
Kote-kote msifuni,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.
6. Sisi na wao pamoja tu
Humo sifani, Humo sifani;
Milele sifa ni moja,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.
Jina Langu Limeandikwa Je
1. Sitafuti mali, wala utajiri;
Nataka kwa yakini nipate Mwokozi.
Chuoni mwa Ufalme, niambie Yesu,
Jina langu yakini limeandikwa, je?
Chorus:
Limeandikwa, je? Jina langu huko?
Kitabuni mbinguni, limeandikwa je?
2. Dhambi zangu ni nyingi, ni kama mchanga,
Lakini damu yako, Mwokozi, yatosha;
Kwani umeahidi; zijapo nyekundu
Zitakuwa nyeupe ilivyo theluji.
3. Mji mzuri sana, wa majumba makuu,
Walipo malaika, mji bila ovu;
Wakaapo walio na mavazi safi,
Limeandikwa sasa, jina langu huko?