Eneza Habari Humu Duniani
Eneza Habari Humu Duniani
Po pote panapo moyo wa huzuni;
Ndimi za Wakristo zitangaze Neno,
Yopo Mfariji.
Ref
Yopo Mfariji, Yopo Mfariji
Roho Mtakatifu, ndiye Msaidizi;
Eneza Habari Humu Duniani,
Yopo Mfariji.
Mfalme wa wafalme, Yesu, umtazame,
Amectuletea siha ya milele;
Mateka wapate Ukombozi wake,
Yopo Mfariji.
Niwezeje mimi kutamka vizuri,
Kumsifu Mwokozi aliye mbinguni?
Nitangaze sasa, neno la furaha,
Yopo Mfariji.
Wenzangu, tuimbe nyimbo za milele,
Mbinguni tujaze na shukrani teLe;
Upendo wa Bwana ujulike sana,
Yopo Mfariji.
Fikira Moja Tu
Fikira moja tu Hurejea tena
Nimekaribia mbingu Zaidi ya jana.
Shika
Karibu na kwetu mbinguni,
Karibu na kwetu sasa,
Nikuone karibu.
Karibu na kwetu Na kwenye makao
Kiti cha enzi cha Mungu, pahali pa mto.
Kamilisha, Yesu, Kuamini kwangu
Nikifika mwisho wangu, Nikuone karibu.
https://youtu.be/5pSgMyac2Ug
Furaha kwa ulimwengu
Furaha kwa ulimwengu, Bwana atakuja!
Kila moyo umpokee,
Viumbe imbeni,Viumbe imbeni, Viumbe vyote Imbeni.
Viumbe imbeni,Viumbe imbeni, Viumbe vyote Imbeni.
Na Bwana atatawala: Watu na waimbe;
Mit, milima na mawe
Kariri furaha, Kariri furaha, Kariri furaha kubwa.
Kariri furaha, Kariri furaha, Kariri furaha kubwa.
Atatawala kwa wema; Atawafundisha
Mataifa haki yake,
Ajabu za pendo,Ajabu za pendo, Ajabu za pendo lake.
Ajabu za pendo,Ajabu za pendo, Ajabu za pendo lake.