Mjini Mwake Daudi
I. Mjini mwake Mfalme Daudi,
Palikuwa zizi nyonge,
Mama alimzaa mtoto
Na horini akamlaza;
Mariamu mama yule
Yesu Kristo Mwana wake.
2. Ni muumba vitu vyote
Alishuka huku kwetu,
Nalo zizi nyumba yake
Na malalo ni majani,
Akakaa na masikini;
Yesu Mkombozi wetu.
3. Na alipokuwa mtoto,
Alimtii mama yake,
Akampenda siku zote
Kwa upendo mwingi sana.
Watu wote wa Kikristo
Wamfuate kwa upole.
4. Maana ndiye mfano wetu,
Alikua kama sisi;
Akajua udhaifu,
Na huzuni na furaha;
Shida na furaha zetu
Yeye anazishiriki.
5. Nasi mwisho tutamwona
Maana ametukomboa,
Mtoto huyu tumpendaye
Ndiye Bwana wetu juu,
Naye ametangulia
Tupafike akaapo.
6. Tutamwona si zizini
Pale ng’ombe wafungwapo,
Tutamwona juu mbinguni
Kuumeni pale Mungu;
Watu wake wamzunguka,
Kama nyota wanang’aa.
Msalaba ndio Asili ya Mema
Sioni haya kwa Bwana,
Kwake nitang’ara!
Mti wake sitakana,
Ni neno imara.
Ref
Msalaba ndio asili ya mema,
Nikatua mzigo hapo;
Nina uzima, furaha daima,
Njoni kafurahini papo.
Kama kiti chake vivyo,
Ni yake ahadi;
Alivyowekewa navyo,
Kamwe, havirudi.
Bwana wangu, tena Mungu,
Ndilo lake jina!
Hataacha roho yangu,
Wala kunikana.
Atakiri langu jina,
Mbele za Babaye,
Anipe pahali tena,
Mbinguni nikae.
Msalabani Pa mwokozi
1.Msalabani pa mwokozi,
Hapo niliomba upozi,
Akaniokoa mpenzi,
Mwana wa Mungu.
Ref
Mwana wa Mungu,
Mwokozi wangu,
Akaniokoa mpenzi,
Mwana wa Mungu.
2.Chini ya mti msumbufu,
Niliomba utakatifu,
Alinikomboa kwa damu,
Mwana wa Mungu.
3.Aliniokoa dhambini,
Ikawa kunikaa ndani,
Aliponifia mtini,
Mwana wa Mungu.
4.Damu ya Yesu ya thamani,
Huniokoa makosani,
Huniendesha wokovuni,
Mwana wa Mungu.
5.Hicho kijito cha gharama,
Leo jivike kwa kuzama,
Kwake uuone uzima,
Mwana wa Mungu.