Kutakuwa Na Baraka
Kutakuwa na Baraka Hiyo ni neon lake
Kutakuwa na furaha Bwana hutoa kwake
Ref:
Baraka nyngi Baraka twahitaji
Tumepokea kiasi Bali twataka nyingi
Kuatakuwa na Baraka Ufufuo twataka
Kwa mabonde na milima Mungu anyeshe mvua
Kutakuawa na Baraka Zitumwagie Bwana
Kuburudishwa twataka Na mvua yako Bwana
Kutakuwa na Baraka Laity zianguke
Haja zetu twaungama Yesu atusikie
Kutakuwa na Baraka Tukimjua na kumtii
Tena tutaburudishwa Tukimpa nafasi
Lo Ajabu Kupata Uzima
Lo! Ajabu kupata Uzima, katika damu ya Mwokozi wangu!
Alinifilia pendoni, Mimi niliyemsulubisha!
Upendo huu wa kushangaza kabisa Wewe Kristo wangu kunifilia pendoni
Upendo huu nashangaa Kristo wangu kunifilia
wangu alitoa damu Siwezi kuelewa neno hili,
Viumbe vyote vya mbinguni Navyo haviwezi kufahamu
Najua tu ni kwa rehema zake Mungu Malaika wote wamsujudu Mungu
Ni rehema tumwabudu, Tumwamini ndiye mwokozi
Aliondoka kule mbinguni Kwa nyumba yake Mungu Baba yake
Na utukufu aliacha Afe kwa ajili ya waovu
Rehema zake ni nyingi na ukarimu Kwani Mungu wangu aliniokoa mimi
Sistahili neema yake, Lakini aliniokoa
Roho yangu ilifungwa sana Dhambi na giza vilinilemea
Ukaniangaza rohoni, Gereza yangu ikaang’aa mno
Ikafunguka minyororo yangu yote Nikaondoka nikaanza kukufuata
Siku ile nitapata Uhuru kweli kwako Mungu
Hukumuni mimi simo sasa Mimi ni wake Yesu ndiye wangu
Yeye ni kichwa changu kweli Na amenivika haki yake
Mimi hodari sasa kwa kiti cha Enzi Napewa taji ya milele katika Yesu
Sina hofu kusogea Katika Bwana wangu Kristo
https://youtu.be/E9Epca0UaG0
Malaika kaleta noeli
Malaika kaleta Noeli ya kwanza,
Kwa wachunga kondoo katika makonde,
Bethlehemu wakawa walinzi wa zamu,
Wakaona usiku ajabu ya nuru
Refrain
Noeli, Noeli, Noeli, Noeli,
Yesu yu Mungu na binadamu
Noeli, Noeli, Noeli, Noeli,
Yesu yu Mungu na binadamu
Wakaona mbinguni, mwangaza wa nyota,
Ing’aayo kwa mbali na masharikini,
Wakaenda upesi, walivyoambiwa.
Bethlehemu wamwone Mwokozi horini
Mashariki watoka wafalme watatu,
Mamajusi waliotafuta mfalme,
Wafuata hii nyota waliyoiona,
Wasipate kumkosa wanayemtafuta
Kiongozi ni nyota iliyowaleta
Hata mji wa Daudi alimozaliwa
Ikakaa mara moja isiendelee
Pale pale nyumbani alimo Mwokozi
Mamajusi walipoingia nyumbani
Wakapiga magoti kwa heshima kuu
Mara hiyo walipozifungua hazina
Manemane, uvumba, dhahabu, watoa