Swahili Hymn N-Z

Nitamshukuru Mungu


Nitamshukuru Mungu,
Kwa upendo wake mkuu,
Alimtuma Mwanawe,
Kunifilia mimi.


Ref
Kweli nitaimba nyimbo,
Za upendo wake mkuu,
Pamoja na malaika,
Walioko mbinguni


Nalifanya dhambi nyingi,
Nilikaa maovuni,
Bali nimeokolewa,
Yesu hunisafisha.


Amenipa Roho yake,
Anijaze daima,
Nimekuwa mwana wake,
Hunipenda kabisa.


Mungu wangu, nashukuru
Husujudu daima,
Neno lako nitangaze,
Kwa upendo popote.

 


Nitembee Nawe


Nitembee nawe Mungu, Alivyotembea Henok;
Mkono wangu uushike; Unene nami kwa upole;
Ingawa njia siioni, Yesu nitembee nawe.


Siwezi tembea pekee; Pana dhoruba njiani;
Mitego ya miguu elfu; Adui wengi hufichwa;
Uitulize bahari, Yesu nitembee nawe.


Ukinishika mkono Anasa kwangu hasara;
Kwa nguvu nitasafiri; “Tautwika msalaba;
Hata mji wa Zayuni Yesu nitembee nawe.

https://youtu.be/pENcA_z-If4

 


Njooni Tumuabudu


1. Njoni na furaha, Enyi wa Imani,
Njoni Bethlehemu upesi!
Amezaliwa mjumbe wa Mbinguni


Ref
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.


2. Jeshi la mbinguni, Imbeni kwa nguvu!
Mbingu zote na zijae sifa!
Sifuni Mungu aliye mbinguni;


3. Ewe Bwana Mwema, Twakubarikia,
Yesu, utukufu uwe wako;
Neno la Baba limekuwa mwili;