Swahili Hymn N-Z

Ni wako Bwana


1. Ni wako Bwana, ninasikia Unaponena nami;
Lakini, kweli, nataka kwako Nizidi kusongea.


Refrain
Bwana vuta, (vuta) nije nisongee
Sana kwako mtini.
Bwana, vuta, vuta, nije nisongee
Pa damu ya thamani.


2. Niweke sasa nikatumike kwa nguvu za neema;
Uyapendayo nami nipende Nizidi kukwandama.


3. Nina furaha tele kila saa nizungumzapo nawe;
Ninanena kama kwa rafiki Nikipiga magoti.

 


Nilikupa wewe


Nilikupa wewe damu ya moyoni,
Ili wokolewe, winuke ufuni.
Nimekunyima ni wewe? Umenipa nini?
Nimekunyima ni wewe? Umenipa nini?


Nilikupa myaka yangu duniani;
Upate inuka, kuishi mbinguni
Nimekunyima ni wewe? Umenipa nini?
Nimekunyima ni wewe? Umenipa nini?


Nimekuletea, huku duniani;
Pendo na wokovu,zatoka mbinguni.
Nimekunyima ni wewe? Umenipa nini?
Nimekunyima ni wewe? Umenipa nini?


Nipe siku zako, Udumu mwangani;
Na taabu yako, wingie rahani.
Nafsi, nafsi, pendo, mali, twae Imanueli.
Nafsi, nafsi, pendo, mali, twae Imanueli.

 


Nimekombolewa na Yesu


Nimekombolewa na Yesu
Aliyenirehemia;
Kwa bei ya mauti yake
Nimekuwa mtoto wake.


Ref
Kombolewa!
Nakombolewa na damu;
Kombolewa!
Mimi mwana wake kweli.


Kukombolewa nafurahi,
Kupita lugha kutamka;
Kulionyesha pendo lake,
Nimekuwa mtoto wake.


Nitamwona uzuri wake,
Mfalme wangu wa ajabu;
Na sasa najifurahisha,
Katika neema yake.


Najua taji imewekwa
Mbinguni tayari kwangu;
Muda kitambo atakuja,
Ili alipo, niwepo.