Swahili Hymn N-Z

Twende Kwa Yesu


1.Twende kwa Yesu mimi nawe, njia atuonya tuijue,
Imo chuoni; na mwenyewe, hapa asema njoo!


Ref
Na furaha tutaiona, myoyo iki takasa sana;
Kwako mwokozi, kuonana, na milele kukaa.


2. “Wana na waje,” atwambia furahini kwa kusikia;
Ndiye Mwokozi wetu hasa, na tumtii, njoni.


3. Wangojeani? Leo yupo: sakiza sana asemapo;
Huruma zake zitwitapo, ewe kijana, njoo.

https://youtu.be/fdRhiwlVpuo

 


Twendeni askari


1. Twendeni askari, watu wa Mungu,
Yesu yuko mbele, tumwandame juu,
Ametangulia Bwana Vitani,
Twende mbele kwani ndiye amini.


Ref
Twendeni askari, watu wa Mungu,
Yesu yuko mbele, tumwandame juu


2. Jeshi la shetani, Likisikia
Jina la Mwokozi, Litakimbia
Kelele za shangwe, Zivume nchini;
Ndugu inueni zenu sauti.


3. Kweli kundi ndogo, watu wa Mungu,
Sisi Na Mababa tu moja fungu,
Hatutengwi nao, moja imani, Tumaini
moja, na moja dini.


4. Haya mbele watu Nasi njiani,
Inueni nyoyo, Nanyi sifuni;
Heshima na sifa ni ya Mfalme,
Juu hata chini, sana zivume.

 


Umechoka Umesumbuka


Umechoka, je, umesumbuka? mwambie Yesu sumbuko lako;
Unayalilia yapitayo? mwambie Yesu pekee.


Refrain
Mwambie Yesu sumbuko lako, yu rafiki amini,
Hakuna rafiki kama yeye, mwambie Yesu pekee.


Je, machozi yakulengalenga? mwambie Yesu sumbuko lako;
Walemewa na dhambi rohoni? mwambie Yesu pekee.


Waogopa shida na majonzi? mwambie Yesu sumbuko lako;
Wasumbukia mambo yajayo? mwambie Yesu pekee.


Kuanzia kifo kukutisha? mwambie Yesu sumbuko lako;
Watamania ufalme wake? mwambie Yesu pekee.

https://youtu.be/v3ACbLT04KU