Swahili Hymn A-M

Jina la Yesu Salamu(Diadem)


1. Jina la Yesu, salumu!
Lisujudieni, Lisujudieni;
Ninyi mbinguni, hukumu,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.


2. Enzi na apewa kwenu,
Wateteea dini, Watetea dini;
Mkuzeni Bwana wenu
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.


3. Enyi mbegu ya rehema,
Nanyi msifuni, Nanyi msifuni;
Mmeponywa kwa neema,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.


4. Wenye dhambi kumbukeni,
Ya msalabani, Ya msalabani,
Kwa furaha msifuni,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.


5. Kila mtu duniani
Msujudieni, Msujudieni;
Kote-kote msifuni,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.


6. Sisi na wao pamoja tu
Humo sifani, Humo sifani;
Milele sifa ni moja,
Na enzi, enzi, enzi, enzi,
Enzi enzi, enzi na enzi mpeni.

 


Jina Langu Limeandikwa Je


1. Sitafuti mali, wala utajiri;
Nataka kwa yakini nipate Mwokozi.
Chuoni mwa Ufalme, niambie Yesu,
Jina langu yakini limeandikwa, je?


Chorus:
Limeandikwa, je? Jina langu huko?
Kitabuni mbinguni, limeandikwa je?


2. Dhambi zangu ni nyingi, ni kama mchanga,
Lakini damu yako, Mwokozi, yatosha;
Kwani umeahidi; zijapo nyekundu
Zitakuwa nyeupe ilivyo theluji.


3. Mji mzuri sana, wa majumba makuu,
Walipo malaika, mji bila ovu;
Wakaapo walio na mavazi safi,
Limeandikwa sasa, jina langu huko?

 


Juu ya mlima uliwekwa mti


Juu ya mlima uliwekwa mti,
Uliodharauliwa. Msalaba huo
Naupenda sana, Hapo Yesu ‘katufilia.


Ref
Naupenda msalaba huu,
Nitashinda kwa nguvu zake.
Naupenda msalaba huu,
Taji nitapewa huko juu.


Msalaba huo naupenda sana, Wengine
Waudharau, Kwani Mwana-Kondoo
Aliacha mbingu, Kutufilia msalabani.


Naona uzuri wa msalaba huu, Damu
Ilipomwagika. Hapo Bwana Yesu alisulibiwa,
Mkombozi wa wenye dhambi.


Nitanyenyekea penye msalaba, Kuyavumilia
Yote. Nitakaribishwa na Yesu mbinguni,
Kwenye utukufu milele.