Swahili Hymn A-M

Furaha kwa ulimwengu


Furaha kwa ulimwengu, Bwana atakuja!
Kila moyo umpokee,
Viumbe imbeni,Viumbe imbeni, Viumbe vyote Imbeni.
Viumbe imbeni,Viumbe imbeni, Viumbe vyote Imbeni.


Na Bwana atatawala: Watu na waimbe;
Mit, milima na mawe
Kariri furaha, Kariri furaha, Kariri furaha kubwa.
Kariri furaha, Kariri furaha, Kariri furaha kubwa.


Atatawala kwa wema; Atawafundisha
Mataifa haki yake,
Ajabu za pendo,Ajabu za pendo, Ajabu za pendo lake.
Ajabu za pendo,Ajabu za pendo, Ajabu za pendo lake.

 


Hakuna Rafiki Kama Yesu


1. Hakuna rafiki kama Yesu, Hakuna, hakuna!
Tabibu mwingine wa rohoni, Hakuna, hakuna!


Ref
Yesu ajua shida zetu;
Daima ataongoza,
Hakuna rafiki kama Yesu,
Hakuna, hakuna.


2. Wakati ambapo hapo yeye, Hapana, hapana!
Wala giza kututenga naye, Hapana, hapana!


3. Aliyesahauliwa naye, Hakuna, hakuna!
Mkosaji asiyempenda, Hakuna, hakuna!


4. Kipawa kama Mwokozi wetu, Hakuna, hakuna!
Ambaye atanyimwa wokovu, Hakuna hakuna!

 


Huniongoza Mwokozi


1. Huniongoza Mwokozi, ndipo nami hufurahi
Niendapo pote napo, ataniongoza papo


Ref
Huongoza, hunishika kwa mkono wa hakika
Nitaandamana naye Kristu aniongozaye


2. Pengine ni mashakani, nami pengine rahani
Ni radhi ijayo yote, yupo nami siku zote


3. Mkono akinishika, kamwe sitanung`unika
Atachoniletea, ni tayari kupokea


4. Nikiishika kazi chini, nitakwenda nako mbinguni
Nako nitamtukuza, Kristu aliyeongoza