Swahili Hymn A-M

Chakutumaini sina

 


1. Cha kutumaini sina,
Ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha,
Dhambi zangu kuziosha.


Ref
Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama.


2. Njia yangu iwe ndefu,
Yeye hunipa wokovu,
Mawimbi yakinipiga,
Nguvu ndizo nanga.


3. Damu yake na sadaka,
Nategemea daima,
Yote chini yakiisha,
Mwokozi atanitosha.


4. Njia yangu iwe ndefu,
Yeye hunipa wokovu
Mawimbi yakinipiga,
nguvu zake ndiyo nanga

 


Chini ya Msalaba


1.Chini ya msalaba Nataka simama;
Ndio mwamba safarini, Wa kivuli chema;
Ni kweli kwa roho yangu Ni tuo kamili,
Tatua mzigo wangu Wakati wa hari.


2.Hapa ni pema sana, Ni ngome kamili;
Hapa yameonekana, Mapenzi ya kweli;
Kama alivyoonyeshwa Yakobo zamani,
Msalaba umekuwa Ngazi ya Mbinguni.


3.Na Yesu msalabani Walimkemea,
Alikufa niokoke Niliyepotea;
Naona ajabu sana Ya mambo mawili
Jinsi alivyonipenda, Nisiyestahili.


4.Atakayeonana, Na Yesu Mbinguni,
Njia yake aanzapo Ni msalabani;
Wokovu upo hapa tu, Mwingine hapana,
Kisha kuna furaha kuu Pamoja na Bwana.


Damu Imebubujika Ni Ya Imanweli


1.Damu imebubujika Ni ya Imanweli
Wakioga wenye taka Husafiwa kweli
Husafi wa kweli, Husafi wa kweli
Wakioga wenye taka Husafi wa kweli


2.Ilimpa kushukuru Mwivi mautini
Nami nisiye udhuru Yanisafi ndani
Yanisafi ndani, Yanisafi ndani
Nami nisiye udhuru, Yanisafi ndani.


3.Kondoo wa kuuawa Damu ina nguvu
Wako wote kuokoa Kwa utimilivu
Kwa utimilivu, Kwa utimilivu
Wako wote kuokoa Kwa utimilivu.


4.Bwana, tangu damu yako Kunisafi kale
Nimeimba sifa zako Taimba milele
Taimba milele, Taimba milele
Nimeimba sifa zako; Taimba milele.


5.Nikifa tazidi kwimba Sifa za wokovu
Ulimi ujaponyamaa Vumbini mwa mfu
Vumbini mwa ufu, Vumbini mwa ufu
Ulimi ujaponyamaa Vumbini mwa ufu.


6.Bwana, umenikirimu Nisiyestahili
Kwa damu yako, sehemu Ya mali ya kweli.
Ya mali ya kweli, Ya mali ya kweli
Kwa damu yako,sehemu Ya mali ya kweli.


7.Nikubali kukwimbia, Mbinguni milele,
Mungu nitakusifia Jina lako pweke.
Jina lako pweke, Jina lako pweke
Mungu nitakusifia Jina lako pweke.